Shule ina madarasa ya kutosha yasiyopungua 12, Ofisi za waalimu, jengo dogo la utawala na vyoo vya kutosha kwa wanafunzi wote.
Pia shule ina mabweni ya kutosha kulala wanafunzi wote wa bweni.
Usalama
Shule ina ulinzi wa hali ya juu. Iko na ukuta mrefu na geti linalolindwa na walinzi. tunakuhakikishia usalama wako na watoto wako.
Usafiri – Basi la shule
Shule inatoa huduma ya usafiri kwa wanafunzi wa kutwa utakaowaleta shuleni asubuhi na kuwarudisha jioni nyumbani. Basi hilo ni la shule lenye ukubwa na kiwango cha kuweza kubeba wanafunzi bila kusongana ndani ya basi.
Gharama zinalipwa kufuatana na umbali wa anakoishi mwanafunzi kutokea nyumbani kwenda shuleni.